Header Ads

MAHAKAMA ZATAKIWA KUJITATHMINI ILI KUTOA MAAMUZI SAHIHI NA YA HAKI KWA JAMII.



PEMBA……. 
                                          
Mkuu wa wilaya ya mkoani Hemed Suleiman Abdalla  amewataka watendaji wa mahakama  kujitathmini katika utendaji  wao wa kazi  kwa lengo la kutoa maamuzi  sahihi  na  ya haki kwa jamii.

Amesema jamii inategemea kupata maamuzi ya haki kwenye chombo hicho , ambapo watendaji wake wanalazimika kujisafisha na kujiepusha na aina yoyote ya udanganyifu au upendeleo.

Ameyasema hayo leo huko ukumbi wa kituo cha huduma za sheria tawi la pemba alipokuwa akiyafungua mafunzo ya siku mbili ya haki za binadamu kwa makadhi na wazee wa mahakama kisiwani pemba .

Amewataka watendaji hao kusimamia haki ipasavyo ili kuifanya jamii kuwa na imani na chombo hicho ambapo pia amewatahadharisha viongozi mbali mbali kujiepusha kuingilia maaamuzi ya mahkama.

Aidha mkuu huyo wa wilaya amesisitiza taaluma ya sheria kusambazwa kwa wananchi vijijini ili kuwa na uwezo wa kuielewa katiba ya nchi na kuepuka matatizo yasiyo ya lazima.

Mapema mratibu wa kituo hicho tawi la pemba Fatma Khamisi Hemed amefahamisha kwamba kituo hicho hakifungamani na upande wowote wa  siasa na kinatoa huduma za kisheria kwa taasisi na makundi mbalimbali ya wananchi bila ya malipo.

Jumla ya mada sita zinazohusu haki za binadamu zitajadiliwa kwenye mafunzo hayo ya siki mbili yaliyotayarishwa na kituo hicho

No comments