CCM YAFANYA UCHAGUZI WA VIONGOZI WA JIMBO.
WILAYA YA MICHEWENI….
Wanachama wa chama cha mapinduzi ccm wametakiwa kuwa na umoja na mashirikiano
ili kuweza kukiletea ushindi chama hicho katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020
Ushauri huo umetolewa na mzee wa chama
hicho Micheweni Ramadhan Shaibu Juma
wakati wa kufungua mkutano wa kuwachagua viongozi wa chama katika jimbo la Micheweni.
Amesema kila kiongozi ana jukumu la
kuwahamasisha wananchi kujiunga na chama cha ccm ili kuongeza nguvu katika uchaguzi
mkuu wa mwaka 2020 na kuwa na wanachama wengi
wenye kuleta manufaa zaidi ndani ya chama hicho.
Akitoa matokeo
katika uchaguzi huo mjumbe wa siasa wilaya ya chake Salama Mbaruku Khatibu amemtaja
Ali Khamis Mbwana kuwa mwenyekiti
kwa kupata kura 36 na kumshinda mpizani wake Shaame Faki Omari aliepata kura 29.
Kwa upande wa katibu aliechukua nafasi
hiyo ni Omari Mwinyi Suwedi na kumshinda
mpizani wake Haji Faki Kombo kwa kupata
kura 16.
Nafasi zilizokuwa zinagombaniwa
katika uchaguzi huo ni wajumbe wa halimashauri kuu ya jimbo ,mkutano mkuu wa jimbo,mkutano
mkuu wa wilaya pamoja na mkutano mkuu wa mkoa na katibu mwenezi.
Hata hiyo baada ya kuchaguliwa viongozi
hao wametakiwa kuendelea kukiimarisha chama ili kiweze kuleta mabadiliko.
Salama amesema viongozi watakapokuwa
makini katika chama wataweza kuleta mabadiliko makubwa na kuweza kuongeza wanachama
wenye uwezo wa kukitetea sehemu yeyote ile.
Post a Comment