Header Ads

KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA CHAZIDI KUTOA ELIMU KWA VIONGOZI NA JAMII.




Pemba.
Viongozi wa dini, viongozi wa serikali za mitaa na wanajamii, kisiwani pemba, wamesema mafunzo ya haki za binadamu, waliopewa na kituo cha huduma za sheria tawi la pemba, yamewapa uwelewa wa mambo mbali mbali ya kisheria, ikiwa ni pamoja na kujua wajibu wao, ndani ya jamii.
Wakizungumza kwenye mkutano wa tathimini uliofanyika kituo cha huduma za sheria mjini chake chake,wamesema kabla ya kupewa mafunzo hayo, hawakuwa na uwelewa huo kwa jamii wanayoizunguka.
Wamesema, kwa sasa wameshawaambia wafuasi wao kuwa, ushahidi wa mtoto, mtu mwenye ulemavu wa kuzungumza na ushahidi wa kielektroniki, unakubalika mahakamani, jambo ambalo awali hawakuwa wakilifahamu.
Sheha wa shehia ya shumba vyamboni wilaya ya micheweni, time said omar, amesema mafunzo hayo nae aliwafikishia wananchi wake, na sasa wapeta uwelewa wa mambo mbali mbali ya kisheria.
Kwa upande wake kiongozi wa kanisa la katolic wete, bibi: anatolia mtawa, amesema waumini wa kanisa lake, wanafahamu vyema maana na katiba na sheria.
Amesema awali akidhani wajibu wake kanisani ni kuwaelezea wafuasi wake, sheria na kanuni za imani ya dini yao, na masuala ya kisheria za nchi hawana wajibu huo.
 Akifungua mkutano huo, afisa mipango wa kituo cha huduma za sheria zaznibar zlsc tawi la pemba, khalfan amour mohamed, amesema kituo baada ya kutoa mafunzo, kinafanya tathmini ili, ili kujiridhisha iwapo mafunzo walioyatoa yamepokelewa.
Amesema, mkutano huo wa tathimini, utawapa dira kwa kujipanga vyema, kwa ajili ya mafunzo mengine yajayo, ili yaweze kufikia lengo lililokusudiwa.
Nae afisa ufuatiliaji na tathmini, kutoka kituo cha huduma za sheria zanzibar, khatib mohamed khatib, amesema ni muhimu mara baada ya kukamilisha mradi, kufanya tathimi ili kujua changamoto na mafanikio yaliofikiwa.
Amesema kituo, kinawaamini wadau wake mbali mbali wakiwemo viongozi wa dini, viongozi wa shehia pamoja na asasi za kiraia, kutokana na kuishi kwao karibu na jamii.
Hata hivyo, afisa huyo amewataka wadau hao wa kituo cha huduma za sheria, kuendelea kuwaelimisha wananchi, juu ya kutambua haki za wajibu wao, na wanapokwama, wasisite kukitumia kituo cha huduma za sheria, kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi.
Kituo cha huduma za sheria zanzibar kwa sasa kimo katika mikutano yake ya tathimini, kwa wadau wake mbali mbali, waliowapa elimu ya sheria na haki za bindamu kwa kipindi cha miaka minne iliopita.

No comments