Header Ads

UNICEF LAIMARISHA HUDUMA ZA USAFI WA MAZINGIRA KOJANI.



PEMBA 

Mkuu wa mkoa wa kaskazini pemba mhe Omar Khamis Othman  amesema misaada inayotolewa na shirika la kuhudumia watoto ulimwenguni (unicef ) imesaidia kuimarika kwa huduma za usafi wa mazingira na kudhibiti magonjwa ya mripuko katika kisiwa cha kojani.

Akizungumza na ujumbe kutoka shirika hilo ukiongonzwa na mwakilishi wake hata nchini bwana ren’e van dangen amesema ujenzi wa vyoo vya kisasa katika kisiwa hicho umesaidia kuimarika hali ya usafi wa mazingira kisiwani humo .

Amesema kabla ya ujenzi wa vyoo hivyo , kisiwani cha kojani kiilikuwa kinara wa ugonjwa wa kipindupindu , ambapo tangu kuanza kutumika wnanchi wamekuwa na elimu sahihi ya kutumia vyoo tofauti na miaka ya nyuma.

Naye mwakilishi wa shirika la unicef tanzania bwana Ren’e Van Dangen amesema shirika lake litaendelea kusaidia sekta mbali mbali za maendeleo ikiwemo afya ili kujenga afya bora kwa watoto .

Ujembe huo pia umetembelea kisiwa cha kojani kuangalia  na kufuatilia maendeleo ya miradi ambayo imefadhiliwa na shirika hilo ambapo wananchi wa kisiwa hicho wameliomba shirika hilo kuongeza msaada wa ujenzi wa vyoo .

No comments