Header Ads

MAPAMBANO DHIDI YA MADAWA YA KULEVYA YAZIDI KUSHIKA KASI.



PEMBA .

Kijana Ali Hamad Salum (32) mkaazi wa Selemu wete amehukumiwa kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 15 au kulipa faini ya shilingi milioni 40  baada ya kutiwa hatiani kwa kosa kupatikana na madawa ya kulevya.

 Hukumu hiyo imetolewa  na  hakimu wa Mahakama ya Mkoa wa Kaskazini Pemba iliyopo Wete, Makame Mshamba  Simgeni.

Ilidaiwa  Mahakamani hapo na mwendesha mashtaka Mohamed Ali Juma kuwa Januari 28, mwaka 2015 majira ya saa 5:00 asubuhi huko kisauni wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba  kijana huyo alipatikana na furushi moja na nyongo nne za bhangi.

Kupatikana na madawa ya kulevya ni kinyume na kifungu cha 15 (1) (a)  cha sheria namba 9 ya mwaka 2009 kama ilvyorekebishwa na na sheria namba 12 ya mwaka 2011 sheria ya kuzuia uingizaji na utumiaji wa mwadawa ya kulevya sheria za Zanzibar.

Kabla ya kusoma hukumu hiyo kijana huyo alipewa nafasi kuiomba mahakama ambapo aliomba mahakama hiyo isimpe adhabu kwa kua hilo ni kosa lake na wakatati alipokamatwa alipigwa na bado hajapoa hivyo kupelekwa chuo cha mafunzo kutamuathiri kiafya.

Hata hivyo ombi hilo limepingwa na upande wa mashtaka na kuitaka mahakama kutoa adhabu kali kwani matendo hayo yamekithiri ili iwe fundisho kwake na vijana wengne wenye tabia kama hizo

Kesi hiyo ilianzwa kusikilizwa kwa mara ya kwanza Machi 11, mwaka 2015


No comments