Header Ads

UTEKELEZAJI WA MAAGIZO YA RAIS WAANZA KUFANYIWA KAZI KASKAZINI PEMBA.



PEMBA.

Serikali ya mkoa wa kaskazini pemba  imeanza kutekeleza maagizo ya mhe rais wa zanzibar kwa kugawa  majukumu ya utekelezaji wa maagizo  hayo kwa maofisa wadhamini wa wizara na taasisi za serikali.

Akizungumza katika kikao cha kutathmini ziara ya mhe rais katika mkoa huo , mkuu wa mkoa wa kaskazini pemba mhe Omar Khamis Othman amewataka kuwa wakweli na wawazi ili kuendana na kasi ya utendaji wa rais kwa kuhakikisha maagizo hayo wanayafanyia kazi.

Amesema kila wizara inapaswa kushiriki katika kusimamia utekelezaji wa maagizo hayo yaliyotolewa na rais wakati wa ziara yake mwezi uliopita katika mkoa huo.

Wakichangia katika kikao baadhi ya maofisa wadhamini wamesema tayari wameanza kuyafanyia kazi maagizo  ya mhe rais kwa kufanya ziara na mikutano ya watendaji wa taasisi zao.

Mapema katibu tawala mkoa wa kaskazini pemba Ahmed Khalid Abdala amewapongeza maofisa wadhamini kutokana na mchango wao uliofanikisha ziara ya mhe rais katika mkoa huo .

Naye mkuu wa wilaya ya wete Rashid Hadid Rashid amewasisitiza wakuu hao wa taasisi kuhakikisha wanawajibika katika kutekeleza maagizo ya mhe rais kwa uwazi ili wananchi wazidishe imani na serikali yao.





No comments