Header Ads

WILAYA YA MKOANI YARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA MIRADI YA MWENGE.



PEMBA.

Mkuu wa wilaya ya mkoani Hemed Suleiman Abdallah ameeleza kuridhishwa kwake  juu ya hatua iliofikia  kwa miradi inayotegemewa  kuzinduliwa na kuwekea mawe ya msingi  katika mbio za mwenge wa uhuru  wilayani humo kwa mwaka huu.

Mkuu huyo wa wilaya  ameyaeleza hayo huko afisini kwake  mara baada ya  kumaliza  ziara  ya  kutembelea maeneo ya miradi yao.

Amesema pamoja na kuridhishwa huko  pia iko baadhi ya miradi  inahitaji  marekebisho madogo madogo,ambapo  amezitaka kamati husika  kufanya marekebisho  hayo  kabla ya  tarehe  20 mwezi huu.

Miradi aliyoitembelea ni pamoja na  nyumba ya madakatari michenzani, soko la matunda na samaki kangani, msitu wa kuotesha mikoko  mwambe na  banda la skuli ya sekondari kengeja.

Miradi mengine ni   kiwanda  cha  kufyetulia matufali  kengeja, kisima cha maji safi  na salama  mahuduthi, mradi wa ufugaji wa ngo’nbe  wa maziwa mgagadu, mradi wa kilimo  mseto  mgagadu na mradi wa ujenzi   wa nyumba ya bei nafuu chambani.

Katika tathmini hiyo pia mkuu huyo wa wilaya  amezungumzia suala  la uokoaji wa zao la karafuu  wilayani humo, ambapo amewataka  wazazi  kutowaruhusu watoto wao  hasa wa kike kushiriki  katika  uokotaji wa  mpeta .

Aidha mkuu huyo wa wilaya  ameitaka jamii  kushirikiana na waalimu  juu ya ushibiti wa utoro wa wanafunzi  maskulini  katika kipindi  hichi  cha  uokoaji wa zao la karafuu.  

No comments