Header Ads

MAPAMBANO DHIDI YA MADAWA YA KULEVYA YAZIDI KUSHIKA KASI.



PEMBA.

Katika mwendelezo wa operasheni wa utokomezaji wa madawa ya kulevya wa Jeshi la Polisi nchini hatimae Jeshi hilo mkoa wa Kusini Pemba jana limefanikiwa kumkamata  kijana mwengine akiwa na jumla ya kete 241 zinazodhaniwa kua ni madawa ya kulevya.

Akizungumza na redio jamii kamanda wa polisi mkoa wa kusini Pemba  Shekhan Mohammed Shekhan amemtaja kijana waliyemkamata kuwa ni Haji Balozi Hassan (35) ambae alikuwa kwenye gari ya abiria akitokea  mkoani kuelekea  micheweni.

Amesema askari walimtilia mashaka abiria huyo ndipo walipoamua kumpekua na kufanikiwa kumkamata na madawa hayo aliyokua nayo katika mifuko yake ya suruali.

Kamanda Shekhan ametoa wito kwa wananchi kushirikiana na jeshi la polisi ili kufanikisha kutokomeza madawa ya kulevya yanayoonekana kuwa ni tatizo katika jamii.

Tukio la kukamatwa Hassan  ni tukio mfululizo wa watuhumiwa wa madawa hayo kukamatwa kisiwani Pemba  ambapo juzi Jeshi hilo lilifanikiwa kumtia mikononi mwanamke mmoja mkaazi wa Wete akiwa na kete 3621 zinazodhaniwa kuwa ni madawa ya kulevya katika maeneo ya mbuguani Mkoani.






No comments