Header Ads

DC MICHEWENI: Ni Marufuku Kusikia Mwanafunzi Kaozeshwa Kwenye Wilaya Yangu


Mkuu wa Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba Bi. Salama Khatibu Mbaruku, akizungumza na Walimu wakuu wa Sikuli za Sekondari Wilayani humo Ofisini Kwake Jana.
mwalimu mkuu wa skuli ya Micheweni sekondari Ismail Ali, akimsikiliza kwa Makini Mkuu wa wilaya wakati wa Kikao Hicho

Baadhi ya Walimu wakuu washiriki wakiendelea kumsikiliza Mkuu huyo wa Wilaya


Walimu Wakuu wakishauriana Jambo na Mkuu wa Wilaya katika Kikao Hicho

Na ali masoud
Walimu katika wilaya ya Micheweni wametakiwa  kutowa ushirikiano katika kupambana na ndoa za mapema ili kuwapa nafasi wanafunzi kusoma masomo yao bila kuwa na vikwazo vya aina yeyote ile

Ushauri huo umetolewa na mkuu wa wilya ya Micheweni  Salama Khatibu Mbaruku wakati alipokuwa akizungumza na walimu wakuuu wa skuli za sekondari  zilizopo wilayani humo

Amesema kuna wanajamii  ambayo wanawaozesha waume wanafunzi  na baadala yake kukosa haki yao ya msingi ya kupata elimu na kukosa wataalamu wa kike

Salama amesema  ndoa za mapema na utoro ndicho kikwazo cha kukosa wataalamu  wa ngazi mbali mbali  ndani ya wilaya hiyo kuahidi suala hilo amelipiga sitopu

“tumejipanga katika wilaya yetu kuhakikisha mitihani yanayotarajiwa kufanyika hivi karibu wanafunzi ambao wameandikishwa  wanafanya kikamilifu”alisema salama

Mkuu huyo wa wilaya amesema atapitia mashule yote yaliyomo wilayani humo ili kujuwa takuwimu za wanafunzi ambao wanahudhuria na wasio hudhuria  ambao wote kupata masomo kama wengine

Hata hivyo mwalimu mkuu mtaaluma  mkasha shame  mbwana amesema wamefurahishwa na kitendo cha mkuu huyo wa wilaya kuwakumbusha wajibu wao ili kuweza kuisaidia jamii

Mkasha ameseama atahakikisha kuwa watakuwa wakibadilishana mawazo na walimu wazke ili kuhakisha watoro na wale ambao wanaolewa na kukatishwa masomo limefikia kikomo

Naye mwalimu mkuu wa skuli ya Micheweni sekondari  Isimali ali ameseme wamejpanga kuhakikisha wanafunzi ambao wanatakiwa kufanya mitihani wanafanya yote bila kuwa na kikwazo cha aina yeyote ile

No comments