Header Ads

Wazalendo Kujenga Mtaro wa Bubujiko Wete



Related imageMKOA WA KASKAZINI PEMBA ..
Serikali Ya Mkoa Wa Kaskazini Pemba Imekutana Na Wataalaamu Wa Ujenzi Ambao Ni Wazalendo Kujadili Ujenzi Wa Mtaro Ulioko Bubujiko Wilaya Ya Wete Na Kuwataka Kuwa Wabunifu Na Watundu Na Kujiamini .

Akizungumza Kwenye Kikao Hicho Mkuu Wa Mkoa Wa Kaskazini Pemba Mhe Omar Khamis Othman Amesema Serikali Inaweza Kupunguza Kutumia Gharama Kubwa Kufuata Wataalamu Kutoka Nje Ya Kisiwa Kazi Ambazo Zinaweza Kufanaywa Na Wataalamu Wa Kizalendo .

Amesema  Ni Vyema Wataalamu Wa Kizalendo Kupewa Nafasi Ya Kuonesha Utaalamu Wao Na Kuwataka  Wajumbe  Na Wakuu Wa Taasisi Zinazoguswa Na Ujenzi Wa Mtaro Huo Kuwatumia Wataalaamu Wa Kizalendo Na Kuacha Kuwatumia Wataalamu Wa Kigeni Ambao Wanatumia Fedha Nyingi .

Naye Mkuu Wa Idara Ya Mipango Miji Pemba Abdalla Salim Amesema Kamati za Kitaifa Na Kamisheni Ya Ardhi Zilifanya Kazi Ya Kukusanya Data , Pamoja Na Kufanya Usanifu Kuutaka Uongozi Wa Baraza La Mji Wete Kufuatilia Ili Kuona Hatua Ambazo Zimechukuliwa .

No comments