Header Ads

DC Mkoani Apambana Kulinda Karafuu



Image result for Shirika la biashara la Taifa ZSTCWILAYA YA MKOANI                        
Kikosi kazi cha usimamizi wa ukoaji wa zao la karafuu kimempongeza Mkuu wa wilaya wa Mkoani na kikosi kazi chake kwa kuendelea kusimamia vyema uokozi wa zao hilo 

Kikosi hicho chini ya mawaziri wasio na wizara maalum Mh Juma Ali Khatib na Mh Said Soud Said  wamesema nia ya Serikali ni kuwalinda wakulima na  wachumaji kwa kuwasaidia kukuza uchumi na kuondokana na umasikini wa kipato 

Kwa nyakati tofauti wameyasema hayo katika ziara yao ya kutembelea kambi na vituo vya kununulia karafuu katika wilaya hiyo.

Mh Juma amesema katika kuona kuwa lengo hilo linafanikiwa amewataka wazazi na walezi kutowaruhusu watoto kuokota mpeta badala yake wawahimize kwenda skuli ili kuwaokoa na vitendo viovu vya udhalilishaji wa kijinsia dhidi yao.

Aidha  waziri Said Soud Said amesema uchumaji katika wilaya hiyo unaitia faraja Serikali kwa kuona unakwendana na ilani ya CCM ya kuinua maisha ya wananchi wake na kuwataka kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuitunza rasilimali hiyo 

Mapema Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman Abdalla amesema tokea uchumaji ulipoanza wamefanikiwa  kuwashajihisha wananchi kuchuma na kuziuza karafuu zao katika shirika la ZSTC

Naye Mdhamini wa Shirika la biashara la Taifa ZSTC Abdalla Ali Ussi amesema kwa ujumla wilaya ya mkoani imenunua tani 1912 zenye thamani ya shilingi bilioni 26 za kitanzania.

No comments