Mawaziri Wasiokuwa na Wizara Maalumu Wawatembelea Wakulima Wa Karafuu Micheweni
![]() |
Waziri asiokuwa na Wizara maalum wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Juma Ali Khatib katika ziara ya kuwatembelea wakulima wa Karafuu Milaya Ya Micheweni kaskazini Pemba wakiwakagua walinzi wa ROAD BLOCK |
![]() |
Waziri asiokuwa na Wizara maalum wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakizungumza na walinzi wa Karafuu-Tumbe, Kutoka Kulia Mbele ni Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mh. Salama Mbaruku Khatibu |
![]() |
Waziri asiokuwa na Wizara maalum wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Juma Ali Khatib akizungumza na wakulima wa karafuu |
![]() |
Msafara wa Mawaziri hao kuelekea kwenye mashamba ya karafuu |
![]() |
Baadhi ya Maafisa Kutoka Afisi ya Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Wakiendelea na Ziara hiyo |
![]() |
Waziri asiokuwa na Wizara maalum wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Juma Ali Khatib Akishuhudia namna wakulima wanavyo dondoa Mpeta |
![]() |
Mkulima wa karafuu akidondoa Karafuu |
MICHEWENI…………26/10
Wakulima wa zao la
karafuu wilaya ya Micheweni wametakiwa kuuza karafuu zao shirika la biashara la
taifa ZSTC ili serikali iweze kuwa na mapato zaidi kwa manufaa ya wananchi kwa
ujumla.
Kauli hiyo imetolewa na
waziri wasiokuwa na wizara maalum wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Juma Ali
Khatib wakati katika muendelezo wa ziara maalum ya kuboresha zao la karafuu
kisiwani pemba.
Amesema kuwepo kwa
vituo vya kuuzia karafuu ni jitihada za serikali ili kuwarahisishia wananchi
kuweza kuuza karafuu zao kiurahisi,na kuwataka kuweza kuvitumia vituo hivyo
kama inavyotakiwa
Naye Said Soud
amevitaka vikosi vya ulinzi na usalama ambavyo vinashughulika na ulinzi wa zao
hilo ikiwemo Road Block kuendelea kulisimamia zao hilo kwa ufanisi waweze
kuliokoa zao hilo la taifa.
Aidha amemtaka afisa
mdhamini ZSTC kuzishughulikia kero zinazowakabili walinzi hao kwa haraka
Naye mkuu wa wilaya ya Micheweni
Salama Khatib Mbarouk amewashukuru mawaziri hao kwa kufanya ziara wilayani
humo, na amewataka wananchi kuziweka karafuu katika sehemu salama hususani
katika msimu huu wa mvua.
Ziara hiyo ya mawaziri
wasiokuwa na wizara maalumu wilaya ya Micheweni ni mwendelezo ya ziara ya
mawaziri hao ya siku nne katika wilaya za kisiwa cha Pemba, ambapo wameweza
kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo.
Post a Comment