Header Ads

Rais Dk. Shein Atumia Salamu Za Pongezi Kwa Wazambia

Image result for RAIS wa Zanziba Mhe. Dk. Ali Mohamed SheinZANZIBAR
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein amemtumia salamu za pongezi Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Changwa Lungu kwa kutimiza miaka 53 tokea Taifa hilo kupata uhuru wake. 

Salamu hizo zimeeleza kuwa wananchi wa Zanzibar wanaungana pamoja na ndugu zao wa Zambia katika kusherehekea siku hii muhimu katika historia ya nchi hiyo ambapo tukio hili la kihistoria lilitokea Oktoba 24 mwaka 1964 ambapo Zambia ilipata uhuru kutoka koloni la Kiengereza.

Aidha, salamu hizo, zimeeleza kuwa tukio hilo kubwa, linatoa nafasi ya kuendeleza uhusiano na ushirikiano mkubwa kati ya nchi mbili hizo hatua ambayo itaimarisha zaidi uhusiano katika nyanja za Kitaifa na Kimataifa yakiwemo mashirikiano ndani ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Afrika (AU) pamoja na Jumuiya nyenginezo za Maendeleo.

Sambamba na hayo, Dk. Shein amemtakia kiongozi huyo pamoja na familia yake na wananchi wote wa Jamhuri ya Zambia, afya njema na kuwatakia sherehe njema zenye amani na utulivu wananchi wa nchi hiyo.

No comments