Header Ads

Wanafunzi Skuli ya Sekondari UWELENI Watakiwa Kujisomea



DSC00013PEMBA
WANAFUNZI wa Skuli ya Sekondari ya Uweleni Mkoani Pemba, wametakiwa kuzidisha nguvu zao katika suala la elimu, ili kuweza kukabiliana na mitihani yao  ya taifa inayotegemewa kuanza mwanzoni mwa wiki ijayo.

Akizungumza na wanafunzi skulini hapo, Mkurugenzi Baraza la Mji Mkoani Rashid Abdalla Rashid, amesema wanafunzi watakapo zidisha nguvu zao katika masomo, wataweza kukabiliana vyema na mitihani yao na kuleta ufaulu mzuri utakaowawezesha kuingia katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi .

Amesema ni vyema kwa wanafunzi hao kujikita katika masomo ya Sayansi, ili waweze kukabiliana na soko la ajira na kupunguza tatizo la uhaba wa madaktari na walimu wa masomo hayo.

Wakati huo huo,  Mkurugenzi huyo ametowa ahadi kwa wanafunzi watakaopata matokeo mazuri ya kiwango cha ‘A’ na ‘B’ ya masomo ya sayansi na kiingereza, kuwazawadia vifaa vya kusomea vikiwemo vitabu mabuku, ada pamoja na sare.

Katika hatuwa nyengine, aliwataka walimu wa Skuli hiyo kusomesha kwa bidii na kuwashajihisha wanafunzi kuachana na masuala yasiyowahusu, ikiwemo kujishirikisha na vikundi viovu.

Kwa upande wake  mwalimu Mkuu wa Skuli hiyo, Shehe Hassan Mohamed amesema, jukumu lililobakia ni la wanafunzi wenyewe kuweza kufanya vizuri, katika kuleta ufaulu  mzuri kwani walimu walikamilisha muhutasari kwa wakati.

No comments