Header Ads

Wazazi Kisiwani Pemba Waaswa Kuto Wasafisha Waathirika wa Udhalilishaji



Image result for Mwendesha mashitaka kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kisiwani Pemba,PEMBA
WAZAZI na walezi nchini, wametakiwa kutowasafisha watoto wao waliobakwa au kulawitiwa, na ikitokezea wamewasafisha, wasisite kuwapeleka hospitali kuwafanyia uchunguuzi.

Kauli hiyo imetolewa na Mwendesha mashitaka kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kisiwani Pemba, Mohamed Ali Juma wakati akijibu hoja za wajumbe wa kamati kuu ya mradi wa GEWE, kwenye mkutano uliofanyika uwanja wa Gombani mjini Chakechake.

Amesema kukosekana kwa maji maji maalum au mbegu za kiume kwenye sehemu iliofanyiwa tendo la ulawiti au ubakaji, hakuuwi kesi, kama wengine wanavyofikiria, na wala ushahidi na ubakaji haondolewi kwa kumuosha mtoto.

Mwendesha mashiataka huyo, ameeleza kuwa hata kama wazazi au walezi watawaosha watoto wao, waliobakwa au kulawitiwa chamsingi wawafikishe hospitalini, kwa ajili ya kufanyiwa uchunguuzi wa kitaalamu, na iwapo wamebakwa njia zake za siri zitaonyesha.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa jamii wilaya ya Wete Haroub Suleiman Hemed, amesema bado wasaidizi wa sheria waliopo majimboni, hawajaibuka vya kutosha kushirikiana na wadau wengine katika mapambano dhidi ya udhalilishaji.

Mratibu wa wanawake na watoto shehia ya Kangagani Awena Salum Kombo, alisema lazima iwepo sheria madhubuti ya kuwaadhibu, wasiotaka kufika mahakamani na kutoa ushahidi.

No comments