Header Ads

Baba wa Kambo Adaiwa Kuwabaka Watoto Watatu Familia Moja KAS PEMBA

Related imagemkoa wa kaskazini pemba  

WATOTO watatu wa familia moja wamefanyiwa kitendo cha udhalilishaji na baba yao wa kambo wenye umri wa miaka 8 , 14 na 16  huku mmoja kati yao akipata ujauzito .
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi watoto hao wamesema kwamba kabla ya kuanza kufanyiwa kitendo hicho na baba yao , alilazimika kupandisha mizuka ambapo shetani aliwataka kuompinga anavyowambia baba yao .
Mmoja wa watoto hao amesema kwamba  baada ya baba yao kumfanyia kitendo hicho alimtaka kutomwambia mama yake na kuahidi kumfanyia kitu kibaya iwapo atatoa taarifa hizo kwa mama yake au mtu mwengine wa karibu yake.
Ameeleza chanzo cha kuanza mahusiano ya kimapenzi na baba yake kilianza zamani na walikuwa wakifanya tendo hilo baada ya mama yake kuondoka ambapo baba huyo alipata fursa ya kufanya naye tendo la ndoa.
Mama mzazi wa watoto hao (jina tunalo) akizungumza na mwandishi wa habari hizi amesema kuwa , baada ya kumuona mwanawe amebadilika kiafya na kumhoji iwapo naujauzito  awali alikana na kudai yuko katika hali yake ya kawaida .
Ameeleza kwamba hali ilimlazimu kumuita dada yake ili amuhoji kwani mabadiliko kimwili  dhidi ya mtoto wake yalikuwa yanaonekana kwamba anaujauzito .
Amefahamisha baada ya kuhojiwa na mama yake mkuu , mshichana huyo alikiri kuwa na ujauzito na kudai kwamba hakuna mwaname mwengine aliyetembea naye isipokuwa baba yake ya kambo ambaye alikuwa akimlea.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Kamishina Msaidizi wa Polisi Haji Khamis Haji amekiri kuripotiwa kwa tukio hilo Ofisni kwake na kusema kwamba jeshi la polisi linaendeela kumtafuta baba huyo ili aweze kufikishwa mahakamani .

Kamanda Haji alifahamisha kwamba mtuhumiwa huyo anaendelea na kutafutwa na Jeshi la polisi na akipatikana atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili .

Naye mratibu wa wanawake na watoto kupitia mradi wa GAWE  katika shehia hiyo Fatma Maulid Salim amesema tukio hilo limemfanya ashirikiane na taasisi mbali mbali ili kudai haki ya watoto hao .
Amesema pamoja na kazi wanayoifanya ya kuielimisha jamii lakini bado baadhi ya wanajamii wanashindwa kutoa ushirikiano na hivyo kusababisha badhi ya kesi kufanyiwa suluhu majumbani.
Kwa upande wake sheha wa shehiya hiyo Omar Khamis Othman amewataka wananchi kuacha kuyafanyia suluhu matendo ya udhalilishaji yanapotokea katika maeneo yao ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua kisheria.

Taarifa ambazo zimepatikana na mwandishi wa habari hizi zinasema kwamba tayari mtuhumiwa huyo amekamatwa na jeshi la polisi kisiwani Unguja na taratibu za kusafirishwa kurejea Pemba kujibu tuhuma hizo .
Mwisho .

No comments