Header Ads

Juhudi kuanza kuchukuliwa uboreshaji Elimu Skuli ya Kizimbani Sekondari


UONGOZI  wa Skuli ya kizimbani sekondari umeanza mikakati ya kuinua kiwango cha ufaulu wa wanafunzi wa kike wa kidato cha nne , kwa kuwaandalia mzaingira mazuri ya kujifunza pamoja na kuwahamasisha wazazi  kushirikiana na walimu kufuatilia maendeleo ya watoto wao.

Hayo yamesemwa na mwalimu mkuu wa skuli hiyo Bisabahi Mussa Said  wakati akizungumza na uongozi wa chama cha mapinduzi CCM Jimbo la gando waliofanya ziara ya kutembelea miradi ya serikali katika jimbo hilo .

 Mwalimu Mkuu wa skuli hiyo Bi Sabah Mussa Said amesema uongozi wa skuli umechukizwa sana na kitendo cha wanafunzi wa kike kufanya vibaya kwenye mitihani ya ya kidato cha nne .
"Mwaka jana wanafunzi wa kike waliofaaulu kuendelea na masomo ya kidato cha tani walikuwa wengi kuliko wanaume , hivyo matokeo ya mwaka huu yametuchanganya walimu ‘’ alisema .

Aidha amesema kuwa moja ya sababu ambazo zimesababisha matokeo hayo ni kwa baadhi ya wazazi kutokuwa tayari kushirikiana na walimu pamoja na kamati ya skuli katika kufuatilia maendeleo ya watoto wao.

Mwenyekiti wa CCM jimbo la Gando Massoud Ismail Juma amesema lengo la ziara  hiyo ni kuangalia utekelezaji wa ilani ya chama pamoja na kufuatilia ahadi za viongozi .

 Mwakilishi wa jimbo la Gando  Maryam Than Juma amewataka walimu kuwa karibu na wazazi kuendelea kushirikiana ili kuwafanya wanafunzi kuongeza uwezo wao kielimu .

Mariam amesema utaratibu wa zamani wa kila mwanafunzi mtoro kuitwa skuli pamoja na mzazi wake unafaa kurejeshwa kwani ni moja ya utaratibu uliokuwa unasaidia wanafunzi kufuatilia masomo yao darasani.

No comments