Header Ads

Korea Kusini na Korea Kaskazini zafungua njia ya simu ya mawasiliano ya moja kwa moja kati ya viongozi wa nchi hizo


Image result for KOREA KASKAZINI RAMANI 
Korea Kusini na Korea Kaskazini zimefungua njia ya simu kwa mawasiliano ya moja kwa moja kati ya viongozi wa nchi hizo mbili.
Mkurugenzi wa idara ya serikali katika Ikulu ya Korea Kusini Yun Kun-young amesema, njia hiyo ya simu imeunganishwa kati ya ikulu ya Korea Kusini na Kamati ya Masuala ya Kitaifa ya Korea Kaskazini.
Rais Moon Jae-in wa Korea Kusini na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un walikubaliana kufanya maongezi yao ya kwanza kwa njia ya simu kabla ya kufanya mkutano wao wa kwanza tarehe 27 mwezi huu katika kijiji cha mpakani cha Panmunjom.

No comments