Header Ads

Umoja wa Afrika wazitaka pande mbalimbali za Sudan Kusini kutimiza ahadi ya mchakato wa amani


Image result for Ujumbe wa baraza la amani na usalama la Umoja wa Afrika PSC 
Ujumbe wa baraza la amani na usalama la Umoja wa Afrika PSC umemaliza majukumu yake ya siku sita nchini Sudan Kusini, ukizitaka pande zote zinazopambana kutimiza ahadi yao kwa mchakato wa amani unaoendelea. 

Ujumbe huo pia umeziaka pande husika kufikiria makubaliano halisi ya amani na kuhakikisha duru ijayo ya mazungumzo ya baraza la HLRF isishindwe kwa kuwa ni fursa ya mwisho kwa amani.
Ujumbe huo umetoa taarifa kuwa ujumbe wa PSC unawahakikishia wadau wote utayari na dhamira ya Umoja wa Afrika ya kufanya juhudi zote katika kuunga mkono IGAD na pande mbalimbali za Sudan Kusini kutatua changamoto zinazoukabili mchakato wa amani.

No comments