NUSU FAINALI ASFC HAPATOSHI LEO KAMBARAGE STAND UNITED vs MTIBWA SUGAR
Kocha wa Mtibwa Sugar, Zuberi Katwila ni mwenye matumaini makubwa
kuelekea kwenye mchezo hyo, akiamimi timu yake itawafunga wenyeji na kwenda
Fainali ya michuano hiyo kwa mara ya kwanza katika historia yao.
Katwila amesema kwamba wachezaji wote muhimu wa Mtibwa Sugar wako fiti
na tayari kwa mchezo wa leo, akiwemo kiungo Hassan Dilunga ambaye alikuwa
majeruhi.
Nusu Fainali ya pili Azam Sports Federation Cup itafuatia Jumatatu
Uwanja wa Namfua mjini Singida, ikizikutanisha JKT Tanzania ya Dar es Salaam na
wenyeji Singida United.
Fainali ya michuano hiyo itafanyika Juni 2, mwaka huu Uwanja wa Sheikh
Amri Abeid mjini Arusha na bingwa pamoja na kupata Sh. Milioni 50, pia
ataiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Mshindi wa pili atapata Milioni 10, wakati Mchezaji Bora atazawadiwa Sh.
Milioni 1 sawa na Kipa Bora, Mfungaji Bora, huku Mchezaji Bora wa Fainali
akiondoka na Sh. 500,000.
Post a Comment