Header Ads

Sh1.5 Trilioni zinazodaiwa kutojulikana zilipo, Serikali yatolea ufafanuzi


Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imesema kuwa, hakuna fedha yoyote ya umma iliyotumika pasi na kuwa na maelezo ya kina juu ya namna fedha hizo zilivyotumika.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Ashatu Kijaji mapema leo bungeni alipokuwa akitoa tamko la serikali kuhusu fedha shilingi trilioni 1.51 zinazodaiwa kutumika bila kuwepo kwa maeneo ya namna zilivyotumika.

Dkt Kijaji amesema kuwa, wale wote wanaozusha kuwa kuna fedha zilitumika bila kuwa na maelezo, hawalitakii mema taifa pamoja na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli.


Akitoa mchanganuo wa matumizi wa fedha hizo Dkt Kijaji alisema, fedha trilioni 1.51 zinazodaiwa kutoonekana kwenye matumizi ya serikali zimetoka na matumizi ya dhamana na hati fungani zilizoiva TZS trilioni 0.6979, mapato tarajiwa TZS trilioni 0.6873, mapato ya kodi yaliyokusanywa kwa niaba ya #ZanzibarTZS trilioni 0.2039. Jumla ya fedha zote hapa inakuwa ni TZS trilioni 1.5891.

Fedha iliyotolewa zaidi ya mapato (Bank Overdraft) ni TZS trilioni 0.0791, na hivyo kufanya kusalia kwa TZS trilioni 1.51 inayodaiwa kutoonekana kwenye matumizi ya serikali.

No comments