Makamo wa Pili wa Rais: 'Wafugaji,wakulima acheni kufanya kazi kwa Mazoea, Fanyeni kwa Malengo

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi amesema wakati umefika kwa Wafugaji wa Samaki
na Mazao mengine ya Baharini Nchini kubadilika kufanya kazi kwa mazoea ya
kupata kitoeo tu, bali wafuge Kibiashara kwa lengo la kuongeza uzalishaji
wa samaki ili kuinua Sekta ya Uvuvi kwa maslahi binafsi, Jamii na Taifa.
Balozi Seif Ali Iddi ameyasema
hayo wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kituo cha Utotoaji wa Vifaranga vya
Samaki {Marine Hatchery} kilichojengwa pembezoni mwa Kampasi ya SUZA iliyopo
Beit - El Ras nje kidogo ya Kaskazini ya Mji wa Zanzibar.
aidha mh Balozi Seif
amefahamisha kwamba mradi wa kutotoa vifaranga vya samaki na mazo mengine ya
Baharini umeanzishwa kwa lengo la kupanua wigo wa shughuli za ufugaji wa samaki
ili Wananchi waweze kuwa na sehemu maalum ya kupata vifaranga vya kutosheleza
na vyenye ubora unaohitajika.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
aliiagiza Wizara ya Kilimo, Mali asili, Mifugo na Uvuvi kuwaandalia mazingira
bora Wananchi wa Unguja na Pemba yatakayowawezesha kupata vifaranga hivyo kwa
urahisi.
Amesema takwimu zinaonysha kuwa zibar
hivi sasa ina zaidi ya Vikundi 144 viavyojishughulisha na harakati za ufugaji
wa samaki ambapo vikundi vyote hivyo hutegemea vifaranga kutoka nje ya Zanzibar
ambavyo havina uhakika wa ubora na upatikanaji wake.
Alieleza kuwa uzinduzi wa Kituo cha
Kutotolea Vifaranga vya Samaki na Mazao ya Baharini cha Beit – El Ras
utakuwa ni ufumbuzi wa changamoto iliyopo kwa Wafugaji wa samaki Nchini hasa
katika upatikanaji wa vifaranga kwa uhakika ambapo kwa sasa wataweza
kuzalisha samaki kwa wingi na kujiongezea kipato.
Alifahamisha kwamba zaidi ya asilimia
50% ya vyakula vyote vya Baharini {SEAFOOD} vinavyotumiwa Duniani hivi sasa
vinatokana na ufugaji, hivyo maeneo ya hifadhi za Bahari ni vyanzo muhimu vya
mazalia ya samaki yanayopaswa kupatiwa hifadhi ya msingi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
aliwaomba Wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar katika uhifadhi wa mazingira ya Bahari kwa faida yao na vizazi
vijavyo.
Mapema akitoa Taarifa Katibu
Mkuu Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Bibi Marya Abdulla Juma
alisema Kituo hicho cha utotoaji wa Vifaranga vya Samaki ni za Barani Afrika
ni cha kwanza cha kumi duniani .
Amesema chuo otoaji wa
vifaranga vya samaki Beit el ras kinatarajiwa kuzalisha vifaranga 10,000 vya
samaki, Kaa 75 pamoja na Majongoo 55 ili baadae kusambaza kwa wafugaji wa mazao
hayo ya baharini.
Akitoa salamu Rais wa Shirika la
Kimataifa la Misaada ya Maendeleo ya Korea {KOICA} Bibi Mikyung Lee aliipongeza
Zanzibar kwa kupunguza ukali wa maisha kutokana na kupiga hatua kubwa za
Maendeleo ikiwemo Sekta ya Viwanda.
Post a Comment