Header Ads

ZAWA yawomba radhi Wananchi, Yasema Tatizo la Upatikanaji wa Maji Safi na Salama linarekebishwa


Image result for MAJI SAFI NA SALAMA 
Afisa  uhusiano   kutoka   Mamlaka  ya  maji  Zanzibar  (ZAWA) amewataka   wananchi   wa  shehia  ya  pete   kuwa  wavumilivu  kutokana na   tatizo  la  ukosefu   wa  maji   safi na salama      kijiji  hapo.

Ameyasema  hayo  Afisa   uhusiano  mamlaka  ya  maji  Zanzibar  (zawa) zahro   Suleiman   kufuatia   malalamiko  yaliojitokeza  kwa  wananchi  kutokana  kwa  kukosekana    huduma  hiyo muhimu katika  katika   shehia   hiyo.

Amesema   kwa  sasa   wamejipanga   kufanya   marekebisho  katika  kisima   cha  maji  kiliopo  unguja   ukuu  kwa  lengo  la  kuwapatia   wananchi  huduma  hiyo.

Kwa upande wa sheha  wa  hiyo  zakia  mbaraka  haji  amekiri  kuwepo  tatizo hilo na    amesema  limeshafikishwa  sehemu  husika    kwa  ajili  ya  kupatiwa   ufumbuzi pia amezungumzia suala la watoto wanaotoka katika kijiji cha pete na kufuata skuli huko  Mtulee.
 
Nae mkazi wa eneo hilo hakupenda jina lake litajwe     amesema   maji  wanayotumia  kwa sasa  ni  ya  kisima  yanayotokana  na  nguvu   za  wananchi   wenyewe  .

Pamoja  na  hayo  mamlaka ya maji zawa imewataka wananchi  kuwa  wastahamilivu kwa kipindi cha   miezi   3 ili  kupatiwa  ufumbuzi wa tatizo hilo.

No comments