' Wadau jitokezeni kukuza Vipaji vya Wanamichezo Zanzibar'

Makampuni
na mashirika binafsi yametakiwa kuunga mkono juhudi za serikali ya Zanzibar
katika kukuza vipaji vya wanamichezo kwa kudhamini michezo mbali mbali ili
kuleta maendeleo ya jamii.
Mkuu wa
mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Ayoub Mohammed Mahmoud ametoa wito huo alipokuwa
akizindua mashindano ya umoja wa shule za sekondari Tanzania kanda ya Zanzibar
katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar ulioambatana na ugawaji wa vifaa vya
michezo vilivyotolewa na kampuni ya Cocacola.
Alisema
serikali kupitia wizara ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar imeanzisha mpango
wa kukuza michezo katika skuli 55 unatambulika kama ‘Sports 55’ uliolenga
kuibua na kuviendeleza vipaji vya wanafunzi wanamichezo ili kutoa matokeo bora
kama ilivyokuwa katika miaka ya nyuma.
Alisema
katika utekelezaji wa mpango huo serikali imejidhatiti kuzalisha walimu,
waamuzi, upatikanaji wa vifaa vya michezo na kujenga viwanja katika
kila wilaya kitakachoweza kutumiwa kwa ajili ya michezo zaidi ya mmoja.
“Toka
ameingia madarakani Rais wa Zanzibar amekuwa akihimiza uwepo wa vuguvugu la
michezo ili kuirudishia nchi yetu (Zanzibar) hadhi yake katika medani ya
michezo jambo ambalo linapaswa kuungwa mkono na kila mmoja wetu katika nafasi
aliyopo”, alisema Mahmoud.
Aidha
Mkuu huyo wa mkoa aliipongeza kampuni ya Cocacola kwa kuamua kudhamini
mashindano ya UMMISETA kwa mwaka wa 3 mfululizo na kuwaasa walimu na wanafunzi
kuvitunza vifaa vilivyotolewa ili viweze kutumika kwa muda mrefu.
“Mnapofanya
hivi sio tu mnasaidia juhudi za serikali katika kuimarisha michezo nchini bali
pia mnajikaribisha kwa jamii kwani hiki mnachokuifanya ni sehemu ya kurudisha
faida mnayoipata kwao kitu ambacho kinapaswa kuzingatiwa na taasisi nyengine”,
alieleza Mahmoud.
Nae
Mkurugenzi wa mawasiliano na matukio kijamii wa kampuni ya Coca cola Haji Mzee
Ally alisema kampuni yake imeamua kudhamini mashindano hayo ili kusaidia
upatikanaji wa viwango bora na wachezaji katika michezo mbali mbali na kkwamba
kampuni hiyo itaendelea kufanya hivyo katika siku za usoni kutokana na kuonesha
kuleta matokeo chanya.
“Tulipoanza
kudhamini haya miaka miwili iliyopita tulilenga kuleta hamasa na mabadiliko
katika sekta ya michezo kitu ambacho tumefanikiwa nacho kwa kiasi kikubwa”,
alisema Haji.
Awali
akitoa taarifa katika tukio hilo, Mkurugenzi wa kamisheni ya michezo na
utamaduni wa wizara ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar Hassan Tawakal
Khayrallah alisema skuli 20 zitapatiwa jezi, viatu na mipira kwa ajili ya
maandalizi ya mashindano ya kanda kabla ili kupata timu zitakazoshirikia
mashindano ya UMISETA taifa yatakayofanyika baadae mwaka huu mjini Mwanza.
Post a Comment