Header Ads

Mkuu wa IMF azitaka Marekani na China kutatua mvutano wa kibiashara kwa kupitia tassisi za pande mbili


Image result for Shirika la Fedha la Kimataifa IMF 
MKURUGENZI mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa Christine Lagarde amezitaka Marekani na China kusuluhisha mvutano wao wa kibiashara kupitia msingi wa kanuni za taasisi za pande nyingi. 

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa kamati ya kutunga sera ya IMF, Bi. Lagarde amesema Marekani na China zinapaswa kufanya kazi kwa msingi wa biashara huria na ndani ya mfumo wa msingi wa taasisi za pande nyingi.

Ushauri wa Bi. Lagarde umekuja wakati waziri wa Fedha wa Marekani Steven Mnuchin akisema kuwa anafikiria kufanya ziara nchini China ili kujadili masuala ya kibiashara na wenzake wa China.

No comments