Header Ads

MSUVA: Nitacheza na SAMATTA


Image result for Simon Happygod Msuva 
WINGA wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Simon Happygod Msuva amekubali kuchezea kikosi cha Marafiki wa Mbwana Ally Samatta katika mechi maalum ya hisani dhidi ya Timu ya mwanamuziki Ali Kiba na rafiki zake kuhamasisha uchangiaji wa vifaa na miundombinu mashuleni Juni 9, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Akizungumza na Vyombo vya habari winga huyo mwenye kasi Msuva amesema kwamba anaunga mkono kampeni hiyo na atakuwepo Juni 9 kucheza mechi hiyo maalum ya Hisani.

Mratibu wa mechi hiyo, Daniel Cleverest amesema kwamba maandalizi yanaendelea vizuri na mgeni rasmi siku hiyo anatarajiwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison George Mwakyembe.

No comments