Header Ads

'Tatizo la Upatikanaji wa Maji kwa Wananchi Micheweni limeisha'

 
TATIZO la uhaba wa Maji linalowakabili wananchi wa Shehia za Majenzi Wilaya ya Micheweni limeanza kutafutiwa ufumbuzi baada ya zoezi la uwekaji wa Mifereji ya Maji na Matanki katika Maeneo hayo kuanza.

Bi Nyota Kombo Rashid, Mmoja wa Wananchi hao akizungumza na REDIO JAMII MICHEWENI amesema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutawapunguzia matatizo wanayokumbana nayo akinamama wa shehia hizo kutokana na uhaba wa Maji.

Sheha wa Shehia hiyo ya Majenzi, Fakh Kombo Hamad, amesema kupatikana kwa mradi huo ni hatua kubwa kwa wananchi wa shehia hiyo kwani wamekuwa wakikabiliwa na Matatizo mbalimbali kwa Mda mrefu.

Mwakilishi wa Jimbo la Micheweni ambae Pia ni Naibu Waziri Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara maaalumu za SMZ Mh. Shamata Shaame Khamis, akishiriki zoezi la Uchumbaji wa Mfereji kwaajili ya kupitisha paipu la Maji Mapema leo.
Akizungumza wakati wa zoezi la uwekaji wa mifrereji hiyo, Afisa wa Maji Wilaya ya Micheweni, Ali Rajab Khalid, amewataka wananchi kuitunza na kuilinda miundombinu hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Awali akizungumza na Wananchi, Mwakilishi wa Jimbo la Micheweni ambae Pia ni Naibu Waziri Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara maaalumu za SMZ Mh. Shamata Shaame Khamis, amesema hatua hiyo ni moja ya juhudi zinazoendelea kufanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kutatua kero za Wananchi wake.

Baadhi ya wanachi walioshiriki zoezi hilo wakiendelea na uchimbaji ma mfereji huo. (PICHA ZOTE NA GASPARY CHARLES- MICHEWENI RADIO)
Mradi huo unaotekelezwa kupitia Halimashauri ya Wilaya ya Micheweni kwa Kushirikiana na Mwakilishi wa Jimbo hilo, umelenga kuelekezwa katika Shehia tatu za Wilaya hiyo ambapo  pia unajumuisha uwekaji wa Matanki ya kutunzia maji pindi maji yanapokuwa hayatoki.

No comments