ZAFELA Walia na Mikataba Umiliki wa Mali kwa Wanandoa Zanzibar

Akizungumza na Jamii
Fm radio Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA,
Jamila Mahmoud amesema hali hiyo inarejesha nyuma
kwa wanawake kufikia malengo yao kwani sheria nyingi
zilizopo sasa ambazo hazijatia mkazo mali za wanawake hasa
wakati wa ndoa zinapovunjika.
Amesema
kesi nyingi zinazopokelewa katika Jumuiya hiyo zinatokana na
wanawake wengi kutokuwa na hati maalum ya umiliki wa mali
pamoja na kuwepo tabia ya kuaminiana bila ya maandishi kwa wanandoa.
Hivyo
amesema ili kukabiliana na tatizo hilo Serikali na Asasi za
kiraia hazinabudi kutoa elimu maskulini na katika jamii
juu ya umuhimu wa kuwepo kwa mikataba ya umiliki wa mali kwa wanandoa.
Jumla ya kesi sita
zilipokelewa katika Jumuiya hiyo kuanzia mwaka jana hadi septemba
mwaka huu ambapo kesi tano zilifikishwa mahakaman na kesi moja imepatiwa
usuluhishi.
Post a Comment