Header Ads

Unaijua Haki yako ya Urithi?.

Related image 
Jamii imetakiwa kuwa na muamko katika kutafuta  hati za umiliki wa mali  mapema  ili kuwapa urahisi watoto kutoingia katika migogoro ya urithi  baada ya wazazi wao kufariki.

Wakizungumza na Micheweni FM  baadhi ya wanawake wa mkoa wa kusini walioshindwa kupata  haki zao baada ya wazazi wao kufariki dunia  kutokana  na kukosa hati za umiliki tangu kwa uhai wa wazazi wao.

Wamesema kutokana na kukosa haki zao mapema imeweza kuleta migogoro kwa familia na kupelekea kushindwa kupata ushahidi  wa kutosha juu ya idadi halisi ya mali zao.

Aidha wamesema licha ya jitihada  wanazozichukua  katika kutafuta haki zao lakini wanashindwa kutokana jamaa zao kutowapa ushirikiano ya kutosha  hivyo wametoa wito kwa wazazi nchini  kuzingatia umuhimu wa kutafuta hati za kumiliki mali mapema kwa lengo la kuwaondoshea usumbufu watoto wao hapo baadae.

No comments