Header Ads

'Viongozi Halmashauri, Baraza la Mji Toeni mrejesho wa Mapato na Matumizi'



Map of Ngezi ForestVIONGOZI wa Halmashauri na Mabaraza ya Miji wametakiwa kujenga utamaduni wa kutoa mrejesho wa mapato na matumizi kwa wananchi jambo ambalo litawajenga imani juu ya utendaji wa kazi  .
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Hifadhi wa Msitu wa Asili Ngezi (NGENARECO) Hassan Suleiman Khamis amesema utafiti uliofanywa na Jumuiya hiyo umebaini kuwa baadhi ya wananchi hawaelewi bajeti za Halmashauri na Mabaraza ya Miji .
Akizungumza na wadau wakati wa uzinduzi   wa Mradi wa Kuhamasisha Uwajibikaji Zanzibar (PAZA) kwenye ukumbi wa mikutano wa Benjamini Mkapa , amesema wananchi wanahaki ya kufuatilia na kuhoji mapato na matumizi hasa wakati huu ambapo Serikali iko kwenye mfumo wa Ugatuzi wa Madaraka .
''Serikali imeshusha madaraka kwa wananchi , hivyo viongozi wa Halmashauri na Mabaraza ya Miji wanapaswa kutoa mrejesho kwa wananchi pamoja na kuweka wazi bajeti zao '' alisisitiza.
Naye Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Mohammed Nassor Salim amesema mradi huo umelenga kuhamasisha sualala uwajibikaji kwa viongozi wa Serikali pamoja na wananchi kushiriki kikamilifu kulinda miundombinu katika maeneo yao.
Amesema imebainika kwamba bado wananchi hawana taaluma na uelewa wa kuilinda miundombinu , na kwamba Mradi huo utahakikisha kwamba kila mmoja anakuwa mlinzi wa miundombinu hiyo.
'' Bado jamii inaonekana kuwa na dhana potofu ya kuona kwamba miundombinu iliyowekwa ,jukumu lakuilinda nila serikali pekee , jambo ambalo linapelekea jamii kushindwa kuchukuliwa hatua  wakati wanaaposhughudia uharibifu '' alieleza.
Mapema akizindua mradi huo kwa Niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa Baraza la Mji Wete , Salma Khamis Juma amewataka wadau hao kuhakikisha wanaihamasisha jamii kushiriki kazi za maendeleo .
Aidha amesisitiza haja lwa viongozi kusimamia vyema majukumu yao ya kazi , na kuwashirikisha wananchi wakati wa kupanga na kuchagua miradi ya kutekeleza .
''Ni vyema kila kiongozi kusimamia kwa uwadilifu shughuli zake za kazi , kwa kuongeza uwajibikaji , ambapo hii itasaidia kuwafanya wananchi kujua kazi zinazzotekelezwa na serikali kupitia Halmashauri na Mabaraza ya Miji '' alisisitiza.
 
Mradi huo wa uhamasishaji uwajibikaji Zanzibar unatekelezwa katika wilaya sita , ambapo kwa Pemba utatekelezwa katika Wilaya ya Micheweni, Wete na Chake Chake .

No comments