Header Ads

'Mahujaji Tafteni Elimu ya Hija kuhimili Hija zenu Saudia'


Image result for mahujaji 
Mahujaji watarajiwa wametakiwa kutafuta Elimu ya hijaa ili kuweza kujuwa nguzo zake na utaratibu wa ibada hiyo kwa lengo la kujiweka sawa kiroho na kimwiliili kuweza kuhimili mazingira ya utekelezaji wa ibada ya hija huko nchini saudi Arabia.

Akitoa semina ya hijja kwa mahujaji watarajiwa huko Baitul amin Malindi Mjini Unguja Ostadh Khalid Mohd Mrisho amesema kua ni lazima mahujaji kujiandaa kiroho na kimwili ili waweze kutekeleza ibadahiyo kwa ufanisi.

Amesema kuwa utakapo pata elimu juu ya ibada ya hijaa utaifanya kwa mazingatio makubwa zaidi na kujitahidi kutafuta kiipato kilicho kuwa halali kwa ibada hiyo.

Aidha mahujaji hao wameelezewa kuwa kufanya ibada hiyo ni kuitikia wito wa Mwenyenzi Mungu kwani ibada hiyo iliaza wakati wa nabii Ibrahimu [as] pale alipo ambiwa walinganie watu watakuja kutoka mjini tofauti.

Hata hivyo ostadh amewataka mahujaji hao kujitarisha katika mambo manene ambayo yataweza kupelekea kukamilika kwa ibada hiyo  kama ilivyo sisitizwa katika Quran.

Nae katibu wa jumuiya hiyo Ali Adam Ali akiwa nje ya semina hiyo anafafanua malengo ya semina hiyokwa mahujaji.

Semina hiyo ya mahujaji inatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku nne mada tofauti zinatarajiwa kutolewa kawa mahujaji hawo lengo kuitambuwa kabla y akufika hulo.

No comments