Header Ads

Wanafunzi Kidato cha Sita Pemba wahimizwa kufuata kanuni za NECTA


Image result for wanafunzi katika mitihani 
KAMATI ya Mitihani Mkoa wa Kaskazini Pemba imefanya ziara na kuzungumza na wanafunzi wanaojiandaa  na mitihani ya kidato cha sita na kuwasisitiza kufuata kanuni na sheria za baraza la mitihani .

Katika nasaha zake kwa wanafunzi hao , afisa elimu na Mafunzo ya amali Mkoa huo mohammed anassor Salum amesema mitihani hiyo inaongozwa na kanuni ambazo zinapaswa kuheshimiwa na kuzingatiwa wakataai wote wa mitihani .

Mohammed amesema baadhi ya masuala  ambayo yamekuwa yakijitokeza kabla na baada ya mitihani ni vitendo vya udanganyifu unafonywa na wanafunzi.

Naye kamanda wa polisi mkoa huo haji khamis haji amewataka wanafunzi kujiepusha na vitendo vya udanganyifu ambavyp vinaweza kuwaharibia malengo yao.

Mwenyekiti wa kamati hiyo bakar ali bakar amesema mwanafunzi akikamatwa na vitendo vya udanganyifu atakuwa anaharibu sifa ya skuli yao .

No comments