Header Ads

Mvua yawakosesha Makazi Watu Saba Wilaya ya WETE


MVUA zinazoendelea kunyesha zimesababisha watu  saba wa familia ya Said Mohammed Salim wa Gando Wilaya ya Wete kukosa sehemu za kuishi  kufuatia  nyumba yao ya kuishi kubomoka baada ya  kuangukiwa na muwembe .

Tukio hilo limelazimu Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Wete ikiongozwana Mwenyekiti wa Kamati hiyo Abeid Juma Ali kufika katika eneo la tukio kwa lengo la kuifariji  familia hiyo .

 Akizungumza katika eneo la tukio Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Wete ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo  Abeid Juma Ali amewataka wananchi kuchukua tahadhari ya kuiondoa  miti ambayo imeshaanza kuoza kwa kufuata sheria ya ukataji miti hasa katika kipindi hichi cha mvua za masika.

Aidha mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa serikali kupitia kamati ya maafa ya wilaya itaangalia uwezekano wa kuisaidia faamilia hiyo hasa katika kipindi hichi na kuwataka kuwa wastahamilivu .

Nae mwathirika wa tukio hilo  Said Mohammed Salim ameishukuru serikali ya wilaya kwa kuwa karibu na wananchi wake jambo ambalo linawawezesha pia kufika katika eneo la tukio kwa wakati.





No comments